Monday 25 April 2016

PENZI LA MVUTO


Umewahi kumpenda na yeye akakupenda?
Kijana mmoja alitokea kumpenda sana dada mmoja japokuwa yeye alikuwa akimtolea nje mara kwa mara lakini kijana hakukata tamaa katika kutafuta bahati yake kwa dada huyo huku akiamini siku moja atafanikiwa. Siku moja dada huyo akiwa yupo nyumbani kwake ikiwa ni siku ya jumamosi tulivu akiwa hajaenda ofisi kwake ambapo alikuwa anafanya kazi katika kampuni moja iliyokuwa inategeneza manukato yenye harufu nzuri mithili ya ua la walidi  aliamua kumpigia simu huyu kaka na kumtaka aje nyumbani kwake, yule kijana alifurahi sana na kuhisi kama ndoto zake zinatimia. 

Akiwa nyumbani kwake dada huyo akifanya shughuli zake ndogo ndogo za hapa na pale alikuwa amevalia kanga moja laini  kutokana na hali ya hewa ya joto la Dar es salaam. Kwa upande wa yule kijana alikuwa amefurahi sana na haraka haraka alijiandaa kwa kuvalia nguo nzuri zenye kuleta mvuto wa mtanashati kisha kuanza safari kuelekea kwa huyu dada njiani kaka huyu alikuwa na mawazo na akijiuliza maswali mengi huku akiwa haamini kama yule dada amemuita nyumbani kwake au ilikuwa ni ndoto. Alipofika, alibisha hodi na yule dada akafungua mlango huku akionyesha tabasamu pana katika paji lake la uso lenye kuleta tamanio la mahaba. 

Yule Kaka aliingia ndani huku kijasho chembaba kikimteremka mithili ya mtu aliyekuwa anakimbia. Dada huyu alimkaribisha vizuri, kisha yule dada akamuuliza anatumia kinywaji gani yule kaka aliitikia kwa upole na ukarimu naomba tu maji ya kunywa huku muda wote akimtazama kwa umakini dada huyu mrembo, aliyeumbika kila idara na ile kanga nyepesi aliyovaa ilikuwa ikionyesha umbo zuri la mahaba liloumbika mithili ya malaika. Kaka alikuwa akivuta pumzi kwa haraka haraka, na kusema "Nimefurahi sana, umenikaribisha nyumbani kwako ni pazuri sana." Yule dada alitabasamu na kusema "Asante sana, nimefurahi pia umeitikia wito wangu, samahani kwa usumbufu wangu".

Yule kaka alitabasamu huku akijisogeza sogeza "Hakuna tatizo, usijali kabisa, mimi nipo kwa ajili yako, naimani sasa nina...." Kabla hajamilizia kuongea yule dada alimshika mikono yake miwili huku akimtizama machoni, kwa macho yake malegevu, mithili ya mtu aliyekula kungu "Samahani kaka, mimi nimekuita hapa kuna jambo nataka unishauri, nataka kujua ni zawadi gani nzuri unaweza kumpatia mwanaume unayempenda" Kaka yule alikuwa akitetemeka na kusema "Chochote tu, zawadi ni zawadi, alimradi kuwe na mapenzi ya kweli" Dada yule alitabasamu na kusema "Ni kweli, mapenzi ya kweli ndiyo jambo la msingi, nitampenda maisha yangu yote" Kaka yule akauliza "Utampenda? Nani huyo"


Yule dada alitabasamu tena na kusema "Samahani, rafiki yangu nilikuwa sijakuambia siku nyingi, wiki ijayo nafunga ndoa na mpenzi wangu wa muda mrefu ambaye nampenda sana, na pia nilikuita ili nikupe kadi ya harusi, nitafurahi kukuona, kwani wewe ni rafiki yangu pia" Yule kaka alibaki amepigwa na butwaa, "Ati, nini unaolewa, daaah, jamani, kwahiyo." Alinyanyuka na kuondoka bila ya kuaga huku akimuacha yule dada anamuita ili ampatie kadi bila ya mafanikio.

Watoto ni Taifa la Kesho tuwalinde

Kengele ya kutoka darasani iligongwa, wanafunzi wa shule ya msingi wakaanza kutoka madarasani huku wakifukuzana wengine wakipiga kelele ilimradi shwangwe tu.Ilikuwa mara yangu ya kwanza kufundisha shule za hatua hiyo. Ilikuwa ni shule ya serikali.
Jicho langu liliangukia katika sura ya msichana mdogo, nguo zake chafu. Alikuwa analia. Alikuwa peke yake na hakuwa na yeyote wa kumbembeleza. Mimi kama mwalimu sikutaka kujisogeza karibu naye sana. Kwanza nilikuwa mgeni. Nikaachana naye.

Siku iliyofuata tukio kama lile likajirudia. Msichana yuleyule wakati ule uleule wa kutawanyika, alikuwa analia sana. Mwishowe aliondoka huku akiwa analia.
“Mbona mwenzenu analia?” nilimuuliza mwanafunzi mmoja.
“Huyo ni mama kulialia..” alinijibu huku anacheka.
Haikuniingia akilini hata kidogo kuwa yule binti analia bila sababu.
Siku ya tatu nikaanza kujiweka karibu naye.
Muda wa mapumziko nilimwita nikamnunulia chai, alikuwa ananiogopa na hakutaka kuniangalia machoni.
Sikumuuliza lolote juu ya tabia yake ya kulia lia kila anaporuhusiwa kurejea nyumbani.

Hata siku hiyo pia alilia vilevile. Wenzake wakawa wanamzomea. Akili yangu iligoma kuamini kuwa binti yule analia bila sababu. Kwanini alie wakati wa kutawanyika tu?? Hapana si bure. Nikaendelea kujiweka karibu naye. Mkuu wa shule akafikishiwa taarifa kuwa nina mahusiano ya kimapenzi na yule mtoto.

Moyo wangu na Mungu pekee ndio walikuwa mashahidi. Nilikosa cha kujibu.
Nilijaribu kujiweka mbali naye lakini moyo ulinambia kuwa kuna jambo natakiwa kulijua. Nikaendelea kuwa karibu naye. Hatimaye mkuu wa shule akanisimamisha kufundisha pale kwa tabia yangu ya kufanya mapenzi na mwanafunzi.

Nilijitetea lakini sikueleweka. Nikamwachia Mungu……
Licha ya kusimamishwa kazi, niliendelea kufuatilia nyendo za yule binti aliyeitwa Janeth. Kila alipotoka shule nilimvizia njiani na kumnunulia chakula, kisha tunazungumza kidogo.
Aliponiamini kama kaka yake ndipo nikajieleza dukuduku langu.
“Janeth…” nilimuita.
“Bee kaka ….” Aliitika huku akinitazama.
“Nyumbani unaishi na wazazi.”
“Ndio naishi na mama..baba huwa anasafiri safari.”
“Mama yako ana watoto wangapi?”
“Mama yangu alikufa….alikufa nikiwa mdogo hata simkumbuki” Alijibu kwa sauti ya chini.
“Kwa hiyo unaishi na mama mdogo.”
“Ndio.”
“Unampenda mama mdogo?”
Swali hili likaikatisha furaha ya Janeth. Akaanza kulia, alilia bila kukoma, Janeth alilia kwa uchungu hadi nikajisikia vibaya. Nilimbembeleza kisha sikumuuliza tena. Siku zikaenda bila kumuuliza chochote..

Baada ya siku kumi, ilikuwa siku ya michezo pale shuleni, hivyo hapakuwa na masomo. Janeth alichelewa kuja shule, nilimngoja uwanjani, hadi alipofika majira ya saa nne.
Nikamwambia twende kunywa chai.
Siku hiyo nilimpeleka mbali kidogo, tukanywa chai, kisha tukakaa mahali palipokuwa wazi. Nikaleta tena mjadala mezani. Ni kuhusu maisha ya Janeth. Alikataa kabisa kusema lolote, nilimshawishi sana. “Usiogope mimi ni kaka yako.” Nilimpooza. Janeth badala ya kusimulia akaanza kulia tena.
“Ataniua mama nikisemaaaa” alilalamika.

Nikambembeleza hatimaye akanieleza jinsi anavyonyanyaswa na mama yake. “Mama hanipendi hata kidogo, ananipiga na kuninyima chakula, hapendi nije shule, vyombo tunavyotumia usiku hataki nivioshe usiku na hataki niwahi kuamka asubuhi, nikiamka natakiwa kufanya kazi zote, kufagia uwanja, kudeki nyumba, kuosha vyombo kisha ndipo nije shule. Baba akiwepo anajidai kunijali sana…”
Alijieleza.
“Ni hayo tu Janeth….niambie kila kitu.”
“Akijua ananiua alisema….”
“Kwani amewahi kukutesa vipi..”
Ni hapa Janeth alivyozungumza huku analia kilio ambacho hakitatoka masikioni mwangu kamwe.
Siku moja, alichelewa kuamka, ilikuwa siku ya mapumziko.
Mama yake alipomwamsha, aliitika na kupitiwa usingizi tena.
Mama aliporejea mara ya pili, alikuwa na mti mkavu, alimpiga nao kichwani na popote pale katika mwili, alipoona hiyo haitoshi akamvua nguo, akausokomeza katika sehemu za siri, aliuigiza hovyohovyo, ukuni huo ulikuwa wa moto.
Yeyote mwenye moyo wa nyama ajifikirie ukuni wa moto ukazamishwa sehemu za siri za mtoto wa darasa la sita.
Nilitokwa machozi.
Nikawahi kujifuta hakuona.
“Baba yeye alisemaje….”
“Baba ni mkali na hapendi kunisikiliza na mama aliniambia nikiambia mtu ananiua mara moja.” Alijibu kwa huzuni.
“Nikija na dada yangu tunaweza kukuona ulivyounguzwa..”
“Ndio…” alinijibu. Sikutaka kulaza damu nikampigia simu rafiki yangu wa kike. Nikamuuliza kama yupo kwake, alikuwepo. Nikaongozana na Janeth.
Tukafika, Janeth akatoa nguo zote.
Ilihitaji moyo wa kiuaji sana kutazama mwili wa Janeth mara mbilimbili. Alitisha, hakika alikuwa ameunguzwa vibaya na vidonda vilikuwa havijapona vizuri. Dada yule alishindwa kujizuia alimlazimisha Janeth twende kwa mama yake amkabiri na kumpa kipigo. Nikamzuia. Hata mimi nilikuwa na hasira kali. Lakini sikutaka kuiruhusu ifanye kazi.
Nikachukua kamera, nikampiga picha Janeth katika yale makovu.

Mbio mbio nikaenda polisi, kituo cha haki za watoto nikaelezea mkasa ule huku nikishindwa kujizuia machozi.
Nikawaonyesha na picha. Tukaongozana nao hadi nyumbani kwao Janeth. Mama yule akakamatwa bila kutarajia. Nilitamani kumrukia nimng’ate lakini haikuruhusiwa.
Sheria ikafuata mkondo. Janeth akaanza kupokea tiba.
Yule mama akahukumiwa kwenda jela miaka sita..hadi sasa yupo jela.
Mume wake alitozwa faini kubwa kwa kosa la kutofuatilia maendeleo ya mtoto wake kiafya…….. Mimi nilirudishwa kazini, kwa heshima kubwa. Heshima ya nkumkomboa mtoto.

***Akina JANETH wapo mtaani kwako…..usiwaangalie na kuwaacha tu…hebu jaribu KUWA SAUTI YAO….hawawezi kusema…hebu sema badala yao…….wanalia kisikie kilio chao.

Saturday 23 April 2016

The need to invest in Africa’s rural transformation

Economic growth remains robust in African countries, but the region has seen a steady rise in the number of extremely poor people, and their concentration in rural areas. 

Two thirds of Africa’s population live and work in rural areas, which offer huge land surfaces, and agriculture represents 65 per cent of jobs in Sub-Sahara.
 

Yet, rural areas have been undervalued by governments, international development lenders and policy advisers. As a result, per capita food production has barely grown over the last 50 years, agriculture only represents 17 percent of Sub-Sahara’s GDP, and its productivity is low and even declining. It’s not surprising that over 60 per cent of rural people live in extreme poverty, and many flee to the cities, where they usually swell the ranks of the unemployed or the informal workforce. 


Boosting agriculture and building around it a strong rural economy is crucial for Africa. Done right, it would create millions of much needed jobs, as well as wealth, inclusion, food security, crisis resilience, and social and political peace. 


This reality is not lost on African leaders. The African Union’s summit held in Addis Ababa on 21-28 January 2014 had as its lead theme “Transforming Africa’s Agriculture: Harnessing Opportunities for Inclusive Growth and Sustainable Development”, and launched 2014 as the Year of Agriculture and Food Security. Participating heads of States and Government adopted a Common Position on the Post-2015 Development Agenda. They also decided to hold a summit in September to review progress achieved since the Ouagadougou Plan of Action was launched ten years ago, and to adopt a roadmap to 2024. Agriculture and rural transformation feature prominently in both the 2004 Ouagadougou Plan of Action and the African Common Position on Post-2015. 

The ILO has actively engaged in rural work since the 1920s, with growing attention to Africa. In 2008, the International Labour Conference adopted a resolution on Rural Employment for Poverty Reduction, which led the way to an ILO Rural Employment and Decent Work Programme (2009-13), and the declaration in 2013 of “Decent Work in the Rural Economy” as an Area of Critical Importance for the Organization. 


The need to recognize the rural potential
A key lesson from ILO rural work is recognizing that rural communities have much potential, and that investment can empower them through integrated approaches. 

This should start with basic physical and social infrastructures such as roads, energy, education and health facilities. Investments should also target relevant skills development and entrepreneurship support, including through cooperatives and innovative financial mechanisms. They should also ensure proper occupational safety and health, social protection and basic rights. 


Many youth are put off by rural jobs that are dangerous, exhausting, badly paid and ill-protected, and by limited infrastructure in rural areas.


Promoting rural areas also means combining agriculture with industrial and service activities to stimulate synergies and diversification, and to seize new opportunities in ICT, tourism, bio-technologies, environment protection and renewable energy generation, for instance.


Integrated approaches also include promoting linkages among public and private stakeholders, developing rural workers’ and entrepreneurs’ structures, encouraging dialogue among them and with authorities, and giving capacities and a voice to youth and women, who are the true engines of rural innovation and growth.

 

All important is disseminating the many winning practices. A good example is the 
Songhaï Centres  in Benin where productive enterprises run activities in farming, processing, handicrafts, marketing, energy production, irrigation, repair, recycling and other services, with strong emphasis on holistic approaches, self-reliance, research and training. The Rwandan Telecentre Network  is another example of good practice, with rural telecentres that provide IT services but are also delivery hubs where individuals, companies and government can advertise, sell, buy and exchange products and services from e-training to banking, insurance, taxation, healthcare, electricity and information. 

“Rural” should become a pivotal part of national and international development agendas. The sense of urgency to tackle agricultural and rural transformation expressed at the African Union Summit augurs well

China rapid economy touch African Rural development

Since initiating market reforms in 1978, China has shifted from a centrally-planned to a market-based economy and has experienced rapid economic and social development. GDP growth has averaged nearly 10 percent a year—the fastest sustained expansion by a major economy in history—and has lifted more than 800 million people out of poverty. China reached all the Millennium Development Goals (MDGs) by 2015 and made a major contribution to the achievement of the MDGs globally.
With a population of 1.3 billion, China recently became the second largest economy and is increasingly playing an important and influential role in the global economy.
Yet China remains a developing country (its per capita income is still a fraction of that in advanced countries) and its market reforms are incomplete. According to China’s current poverty standard (per capita rural net income of RMB 2,300 per year in 2010 constant prices), there were 70.17 million poor in rural areas in 2014.   
Rapid economic ascendance has brought on many challenges as well, including high inequality; rapid urbanization; challenges to environmental sustainability; and external imbalances. China also faces demographic pressures related to an aging population and the internal migration of labor.
Significant policy adjustments are required in order for China’s growth to be sustainable.  Experience shows that transitioning from middle-income to high-income status can be more difficult than moving up from low to middle income.
China’s 12th Five-Year Plan (2011-2015) and the newly approved 13th Five-Year Plan (2016-2020) forcefully address these issues. They highlight the development of services and measures to address environmental and social imbalances, setting targets to reduce pollution, to increase energy efficiency, to improve access to education and healthcare, and to expand social protection. The annual growth target in the 12th Five-Year Plan was 7 percent and the growth target in the 13th Five-Year Plan is 6.5 percent, reflecting the re-balancing of the economy and the focus on the quality of growth while still maintaining the objective of achieving a “moderately prosperous society” by 2020 (doubling GDP for 2010-2020). 
  

Lessons from EU framework for rural development programmes for Rural Tanzania

The EU’s rural development policy helps the rural areas of the EU to meet the wide range of economic, environmental and social challenges of the 21st century. Frequently called "the second pillar” of the Common Agricultural Policy (CAP), it complements the system of direct payments to farmers and measures to manage agricultural markets (the so-called "first pillar"). Rural Development policy shares a number of objectives with other European Structural and Investment Funds (ESIF).

Member States and regions draw up their rural development programmes based on the needs of their territories and addressing at least four of the following six common EU priorities:
  • fostering knowledge transfer and innovation in agriculture, forestry and rural areas;
  • enhancing the viability and competitiveness of all types of agriculture, and promoting innovative farm technologies and sustainable forest management;
  • promoting food chain organisation, animal welfare and risk management in agriculture;
  • restoring, preserving and enhancing ecosystems related to agriculture and forestry;
  • promoting resource efficiency and supporting the shift toward a low-carbon and climate-resilient economy in the agriculture, food and forestry sectors;
  • promoting social inclusion, poverty reduction and economic development in rural areas.
The rural development priorities are broken down into "focus areas". For example, the priority on resource efficiency includes focus areas "reducing greenhouse gas and ammonia emissions from agriculture" and "fostering carbon conservation and sequestration in agriculture and forestry". Within their RDPs, Member States or regions set quantified targets against these focus areas. They then set out which measures they will use to achieve these targets and how much funding they will allocate to each measure. At least 30% of funding for each RDP must be dedicated to measures relevant for the environment and climate change and at least 5% to LEADER

Friday 22 April 2016

175 nations sign historic Paris climate deal on Earth day

World leaders from 175 countries signed the historic Paris climate accord Friday, using Earth Day as a backdrop for the ceremonial inking of a long-fought deal that aims to slow the rise of harmful greenhouse gases.

"We are in a race against time." U.N. secretary-General Ban Ki-moon told the gathering at the United Nations headquarters in New York. "The era of consumption without consequences is over."

"The poor and most vulnerable must not suffer further from a problem they did not create," Ban added.

U.S. Secretary of State John Kerry signed the document while holding his young granddaughter. She was one of 197 children at the event to represent the parties that adopted the agreement, Ban said.

"These young people are our future. Our covenant is with them," Ban said. "Today is a day for our children and grandchildren and all generations to come."

Image result for paris climate agreement

The non-binding treaty, approved in Paris in December after years of U.N. climate negotiations, aims to slow the rise of greenhouse gases, such as carbon dioxide, blamed for putting Earth on a dangerous warming path.

The deal sets a target of limiting global warming by 2100 to “well below” 2 degrees Celsius (3.6 degrees F), as compared to pre-industrial levels. To accomplish that, each nation sets its own target for reducing emissions and updates that mark each year.

Friday's signing sets a record for the number of countries signing an agreement on the first available day, the Associated Press reported. The old record goes back to the Law of the Sea in Montego Bay, which was signed by 119 countries in 1982, according to Accu Weather.

Maarifa Ni Ufunguo- Use of teaching Locally made materials in ECD

Maarifa Ni Ufunguo- ECD Teachers training

Christina Shusho - Ninanga'ra Official Music Video

REA YAELEZEA MAENDELEO YA MFUKO WA NISHATI VIJIJINI

Rural Development- An Integrated Concept of Growth and Poverty Elimination

Mobisol Na maendeleo Vijijini Tanzania

Ushirikiano kati ya Serikali na taasisi mbalimbali zenye lengo la dhati katika kutatua changamoto na kero mbalimbali katika maisha ya wananchi hasa  vijijini ambayo upatikanaji wa huduma za kijamii kama umeme ni ghali ukilinganisha na kipato chao ni muhimu sana kwa tija na maendeleo ya wananchi. Kama mdau na mtaalamu wa maendeleo vijijini napenda kuipongeza kwa dhati kabisa kampuni ya Mobisol Tanzania ambayo inahakikisha kuna maisha bora na yenye kuleta tija kwa wananchi wa Tanzania 

"Mobisol inatoa nishati safi na salama kwa maelfu ya jamii za vijijini zisizo na nishati ya uhakika"


Kwa mipango yake pamoja na ule wa Serikali yetu tukufu ya awamu ya Tano kupitia wizara ya Nishati na Madini chini ya Waziri Prof Sospeter Muhongo kupitia idara ya Umeme vijijini (REA) hakika tunaiona Tanzania mpya yenye Maendeleo endelevu kuanzia vijijini hadi mjini.
Hebu pitia japo kwa ufupi mafanikio ya Mobisol kwa Tanzania   http://www.mobisol.co.tz/ 
Kampuni ya Mobisol yenye makao yake makuu mjini Berlini nchini ambayo inajihusisha na uzalishaji wa umeme wa jua tayari imewaunganisha wateja wapatao 30,000 nchini Tanzania katika kipindi cha miaka 2 tangia ianze kutoa huduma hizi barani Afrika.
Kasi hii ya ongezeko la wateja wanaotumia umeme nishati ya jua kutoka kampuni hii inadhihirisha kuwa uwekezaji wake unaendana sambamba na kuunga mkono jitihada za serikali ya Tanzania za kupunguza tatizo la upatikanaji nishati ya umeme nchini.
Katika kuadhimisha mafanikio ya kufikisha idadi ya wateja 30,000 Mobisol imetoa msaada wa kuinganisha na umeme wa nishati ya jua zahanati ya serikali ya kijiji cha Ngasamo kilichopo Simiyu ambapo anatokea mteja aliyejiunganisha na umeme wa kampuni hiyo akiwa anakamilisha idadi ya wateja 30,000 katika nchi hizi mbili za Tanzania na Rwanda ambako inatoa huduma zake.
Akiongea wakati wahafla ya kutoa msaada huo iliyofanyika katika zahanati hiyo, Meneja Masoko wa Mobisol Bwana Nkora Nkoranigwa amesema kuwa kampuni hiyo imejizatiti kuondoa tatizo la giza nchini na kuaikisha iawapatia wananchi umeme wa nishati ya jua wa uhakika kwa kutumia teknolojia ya kisasa na gharama nafuu.

“Sote tunaelewa kuwa nishati ya umeme inahitajika katika kuleta maendeleo ya haraka na kuwaongezea vipato hususani wakazi wa vijijini.Tutahakikikisa tunaunga mkono jitihada za serikali za kuzalisha na kusambaza umeme kwa kwa wananchi hususani wanaoisi maeneo ya vijijini kwa gharama nafuu ii uwasaidia katika itihada zao za kujiendelea kimaisha” alisema.
Bwana Nkoranigwa alisema umeme ikipatikana utasaidia wananchi kuachana na matumizi ya vibatari na kufurahia matumizi ya vifaa vya kisasa kama jokofu, feni, kuchaji simu na viginevyo na kuwezesha watoto kujisomea katika mazingira mazuri wawapo majumbani na mashuleni hali ambayo itasaidia kuongeza kiwango cha ufaulu katika masomo yao.
30000
Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Bwana Patrick Onyango alishukuru kwa msaada huo na kusema kuwa utawaondolea kero ya kukosa nishati ya umeme waliokuwa nayo kwa muda mrefu na itarahisisha utoaji wa huduma za matibabu kwa wagonjwa na aliahidi kuwa watahakikisha wanatunza vizuri vifaa vya nishati hiyo walivyozawadiwa “Kuna msemo kuwa akufaaye kwa dhiki ndio rafiki wa kweli”. Tunaishukuru kampuni ya Mobisla kwa msaada huu wa kusaidia wananchi wengi” alisema.
Naye Afisa Utawala wa Wilaya hiyo kwa niaba ya serikali alishukuru kwa zahanati hiyo kupatiwa msaada wa nishati na aliongeza kuwa serikali wilayani humo itazidi kuunga mkono wawekezaji wanaokuja na miradi ya kusaidia kuleta maendeleo katika jamii kama ulivyo mradi wa nishati wa Mobisol.
Kwa upande wake mteja wa 30,000 wa kampuni ya Mobisol ambaye alisababisha hafla hiyo kufanyika kijijini hapo na zahanati kupatiwa msaada alisema kuwa amefurahi kuona kampuni memuenzi kwa kuleta msaada wa nishati kwenye zahanati wa kuwanufaisha wananchi wote. Akiwa ni mteja wa umeme unaozalishwa na kampuni hiyo alisema ni wa uhakika na gharama nafuu na unafanya maisha kuwa rahisi na kisasa na kuwataka wanakijiji wajiunge kwa aili ya kuishi maisha ya kisasa na kuweza kuanzisha miradi midogo midogo ya uzalishaji kwa utumia nishati hiyo
Chanzo: http://www.mobisol.co.tz



Monday 18 April 2016

RAIS AMTEUA MATHIAS CHIKAWE KUWA BALOZI NCHINI JAPANI

IKULU

Daraja la Kigamboni Fursa kwa Tanzania Mpya

Tukizungumzia Daraja Bora lenye mvuto wa aina yake katika nchi zote za Ukanda wa Afrika Mashariki hutaacha kulitaja Daraja la Kigamboni linalopatikana Dar es Salaam Tanzania pekee lakini kubwa zaidi ndio Daraja pekee linalopita juu ya maji.
Daraja hilo limetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya matumizi ya kamba (Cable) kubeba uzito wa daraja, ambalo linaunganisha jiji la la Dar es Salaam na eneo la Kigamboni na Kurasini.
Pamoja na kujengwa katika ubora wa hali ya juu, daraja hili lina jumla ya njia sita yaani njia tatu kwa kila upande, pamoja na njia mahususi kwa ajili ya waenda kwa miguu na waendesha baiskeli ambayo ina upana wa mita 2 na nusu (2.5 meters) katika kila pande likiwa na uwezo wa kupitisha magari yenye uzito usiozidi tani 30.
Watanzania wanajivunia kuwa na daraja zuri, la pekee Afrika ya Mashariki linalopita baharini lenye kuvutia kutokana na muonekano wake hasa nyakati za usiku.
Hadi kukamilika kwa ujenzi wake Daraja la Kigamboni limegharimu kiasi cha dola milioni 135 sawa na shilingi bilioni 283 likitazamiwa kuzinduliwa rasmi Aprli 19 na Rais Dk. John Magufuli.
Mambo muhimu ambayo madereva na watumiaji wengine wa barabara wanatakiwa kuzingatia ni:-
1) Kuzingatia sheria ya Usalama Barabarani ikiwa ni pamoja na kufuata mwendo kasi unaotakiwa ili kuepuka ajali na kuepuka uharibifu miundombinu ya daraja
2) Kufuata alama za barabarani zilizowekwa katika ‘Interchange’ ya Kurasini ili kwenda kwenye uelekeo sahihi.
3) Kuzingatia alama zilizowekwa kwenye milango (Toll Gates) ya Kituo cha kulipia tozo (Toll Plaza) ili kuepuka uharibifu wa miundombinu ya kituo hicho.
4) Madereva na watumiaji wa barabara wengine watakaosababisha uharibifu wa aina yeyote wa miundombinu ya daraja watatozwa faini au kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria.
5) Kutunza mazingira kwa kuepuka kutupa takataka katika eneo la daraja.
DARAJA LA KIGAMBONI (2)
Aidha, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inawataka madereva wa magari ya mizigo wanaoegesha katika barabara ya Nelson Mandela wakisubiri kuingia bandarini watafute eneo stahiki la maegesho na kuyaondoa magari hayo kwani hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale watakaoenda kinyume na agizo hili.
Msongamano wa magari hayo husababisha uharibifu wa barabara na usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa barabara katika eneo hilo.



Monday 11 April 2016

Kwa nini Ndoa za Sasa hazidumu?

NI siku nyingine tena mpenzi msomaji tunakutana kwenye uwanja wetu wa kupeana mada mbalimbali zenye ujumbe wa masuala ya uhusiano na ndoa.
Ni ukweli usiopingika kwamba siku hizi ndoa nyingi hazidumu. Watu wanaoana kwa mbwembwe nyingi lakini ndani ya miezi kadhaa, mwaka mmoja au miwili, wanaachana. Ukifanya utafiti wa kina utakutana na sababu mbalimbali zinazosababisha tatizo hilo.
Ukirudi katika historia utagundua kwamba, kizazi kile cha ndoa zilizofungwa miaka ya tisini kurudi nyuma, kilikuwa tofauti. Ndoa zilifungwa na kudumu kwelikweli.

Suala la msingi hapa la kujiuliza ni kwa nini ndoa za sasa hazidumu? Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo lakini kwenye makala haya tutazijadili chache ili mwisho wa siku kila mmoja wetu, aangalie kitu cha kufanya ili kuhakikisha anaingia kwenye ndoa salama na itakayodumu.

Utandawazi ni suala ambalo kwa kiasi kikubwa limechangia kuharibu maadili ya Watanzania wengi wamekuwa wakiiga maadili ya nchi za Magharibi na kuyaweka katika mazingira ya  ndoa zetu. Mfano; mtu anafuata utamaduni ambao pengine unaruhusu mapenzi ya jinsi moja.
Anapokutana na mwenzake ambaye utamaduni huo hakubaliani nao, moja kwa moja ndoa yao itakuwa na migogoro ambayo mwisho wa siku huishia kuvunjika. Pia kutokana na utandawazi huo,

watu wamegeuza ndoa kuwa ni kama fasheni. Kwamba anaweza akaoa leo, kesho akaachana na mwenzake. Anaweza akaoa tena kulingana na mahitaji yake kwa wakati huo. Hachukulii kwa uzito suala la ndoa akiamini kwamba hata akiachana na mkewe, hawezi kuwa wa kwanza. Wengi tu wameshaachana.

Maadili
Kizazi cha sasa kimepotoka kimaadili. Wengi wanafikiri ujanja ni kuishi kama wenzetu Wazungu. Wanawake na wanaume wanaamini kuvaa nguo za ‘mitego’ ndiyo chambo cha kunasa wapenzi.
Mwanamke anaolewa lakini bado anataka atamaniwe na watu. Anajirahisisha bila hofu kwamba utayari wake unaweza kusababisha maafa katika ndoa.

Yupo tayari tu ndoa ivunjike. Anaona hakuna cha kupoteza. Anaamini yeye ni bidhaa adimu. Inayoweza kuuzika wakati wowote. Kwamba anaweza kuachwa, ndani ya muda mfupi atapata ‘mteja’ mwingine ambaye ataendeleza jahazi la mahitaji ya ndoa.
Hofu ya Mungu Kizazi cha sasa kimemsahau Mungu. Hakina hofu ya Mungu. Suala hili limechangiwa pia na wazazi. Wameshindwa kuwajengea misingi imara katika ngazi ya chini matokeo yake wanawashindwa. Mzazi anaweza kuwa na maadili mazuri, anakwenda msikitini au kanisani, ana hofu ya Mungu lakini mtoto wake hana.
Tamaa
Kizazi cha sasa kimeharibiwa na utandawazi. Mtu anaingia kwenye ndoa si kwa sababu ya mapenzi ya dhati. Anaongozwa na tamaa ya mwili. Matokeo yake anakutana na mtu ambaye si sahihi. Wataingia kwenye ndoa, watajikuta wanagombana na  baadaye wanaachana.
Nini kifanyike? Kwa yeyote anayetaka kuingia kwenye ndoa anapaswa kuingia bila tamaa za kimwili. Aangalie tabia njema ya mwenzake. Aaangalie kama mwenzake ana hofu ya Mungu.