Wednesday 30 April 2014

Lishe asili ni dawa ya wagonjwa wa moyo


Kula vyakula asili inazidisha miaka ya wagonjwa wa moyo Wanasayansi nchini Marekani wanasema watu waliowahi kupata maradhi ya moyo wanaweza kuishi maisha marefu iwapo watakula zaidi vyakula ambavyo havijapitia viwandani.
Watafiti walichunguza zaidi ya watu elfu nne waliowahi kupata mshituko wa moyo na kubaini kuwa wana uwezekano mkubwa wa kuishi miaka tisa zaidi kama watakula vyakula hivyo .

Vyakula ambayo havijapitia viwandani vina nyuzinyuzi ambazo tayari imethibitishwa kuwa husaidia katika kuwezesha binadamu kwenda haja bila matatizo.

Vyakula ambayo vina nyuzinyuzi hizo ni kama vile matunda, mboga na nafaka.
Hatahivyo wataalam wanasema watu katika mataifa mengi hawali vyakula hivyo kwa wingi.

'Wezi kukatwa mikono na wazinifu kupigwa mawe'


 
 
Sultani na mtawala wa Brunei ambaye ni mmoja wa matajiri wakubwa duniani Serikali ya Brunei iliyo Kusini Mashariki mwa Bara Asia, itaanza kutumia sheria kali za kiisilamu.
Kiongozi wa nchi hiyo ya kiisilamu ambayo ni jirani na Malaysia ametangaza kuwa sheria hiyo itaanza kutumika kuanzia wiki hii.

Adhabu zilizo chini ya sheria za kiisilamu ni pamoja na kuwakata wezi mikono na kuwapiga mawe hadi kufa watu waliopatikana na hatia ya kushiriki Zinaa.
Sheria hii itatekelzwa katika awamu tatu katika kipindi cha miaka mitatu. Umoja wa Mataifa tayari umeelezea wasiwasi wake kuhusu sheria hiyo.

Taifa la Brunei tayari linafuata sheria kali za kiisilamu kuliko hata nchi jirani kama Malaysia na Indonesia pamoja na kuharamisha uuzaji na utumiaji wa pombe.
Nchi hiyo ndogo ilio katika kisiwa cha Borneo,inatawaliwa na Sultan Hassanal Bolkiah na imepata utajiri wake kutokana na kuuza nje mafuta na gesi yake.

Takriban nusu ya waisilamu wanaoishi katika nchi hiyo ni raia wa Malaysia.
Sultani alinukuliwa akitangaza hatua ya kwanza ya kuanza kutumiwa kwa sheria hiyo akimshukuru Mungu na kuwatahadharisha wananchi kuhusu kuanza kutumika kwa sheria hiyo.

Sheria yenyewe itaanza kutumika katika kipindi cha miaka mitatu huku hukumu ya makosa ya kwanza ikiwa kifungo cha jela pamoja na kutozwa faini.

Katika awamu ya pili ndipo wahalifu wataanza kukatwa mikono kwa watakaopatikana na hatia ya wizi , huku awamu ya tatu ikihusu kupigwa mawe wazinifu na wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja.

Sultani anayetawala kisiwa hicho ni mmoja wa matajiri wakubwa duniani na tayari amewaonya watu kukoma kushambulia mipango yake kupitia mitandao ya kijamii.
Mfumo wa sheria katika mahakama nchini humo ni sawa na ule wa Uingereza.
Umoja wa Mataifa uliitaka serikali kuchelewesha mageuzi hayo ili kuhakikisha kuwa sheria hiyo inaambatana na sheria za kimataifa kuhusu haki za binadamu.

 source: BBC Swahili

Monday 28 April 2014

Friday 25 April 2014

FAHAMU AINA KUMI (10) ZA WANAWAKE WANAOPENDWA ZAIDI NA WANAUME

WENYE MSIMAMO

Wanawake daraja la kwanza wanaopendwa zaidi na wanaume ni wale wenye msimamo, uelewa mkubwa wa mambo na maamuzi sahihi, walio makini kwenye matendo yao na siku zote hufanya vitu kwa ajili ya kupata mafanikio. 
 
WAPENDA USAWA
 Aina ya pili inayohitajika katika katika ulimwengu wa kimapenzi ni wanawake wanaoheshimu usawa wa jinsia, walio tayari kubeba majukumu ya kifamilia kwa ulinganifu sawa na wanaume, wenye uwezo wa kuongoza jamii kwa asilimia 50 kwa 50. 

WANAOJUA MAPENZI 
Wanawake wajuzi wa mambo ya faragha wanapendwa sana. Sifa yao kubwa ni uwezo wa kuwatosheleza wenzi wao katika tendo la ndoa. Tafiti zinaonesha kuwa wanaume hupenda sana wanawake watundu katika mchezo wa sita kwa sita. Mara nyingi wanatajwa kuwa na uwezo wa kuteka akili za wanaume bila kujali sifa zao za nje au za ndani.

MARAFIKI 
Wanawake wenye sifa sawa na rafiki ni aina ya nne inayowavutia wanaume. Wao hutegemea zaidi nguvu ya kushawishi inayotokana na namna wanavyojali na kujitolea kuhakikisha wanakuwa marafiki wa kweli kwenye shida na raha kwa wapenzi wao. Si wakorofi, ni waungwana na wapenda amani. 

WAPENDA UWAZI 
Aina nyingine ya wanawake inayowavutia wanaume ni wenye msimamo na wapenda uwazi. Si wepesi wa kuburuzwa katika maamuzi ya msingi kwa kisingizio cha wao ni wanawake. Utafiti unaonesha wanawake wa aina hii wamekuwa muhimu hasa kwa wanaume wenye tabia za ubabe na udhaifu katika uelewa wa mambo. 

WANAOJITEGEMEA  Wanawake wanaojitegemea wana soko kubwa kwa wanaume tofauti na akina ‘naomba vocha’ kila siku. Uchunguzi unaonesha kuwa wanaume wa leo hawapendi wanawake tegemezi, wasiokuwa na kazi na wanaoendekeza starehe za upande mmoja. WASIO NA PRESHA Nikisema wanawake wasiokuwa na presha namaanisha wasiolazimisha vitu vitokee haraka haraka. Wao siku zote huacha mambo yatokee yenyewe na kazi yao kuwa ni kutenda sehemu ya majukumu yao kama wapenzi. 
 
MARIDADI  Kundi lingine la wanawake wanaopendwa na wanaume ni wanaozingatia usafi na kujiremba. Wanaokwenda na wakati katika mavazi na mvuto wa nje lakini pia ni waelewa wa mazingira, si washamba. Wanapendeza kwa mwonekano. WANAORIDHIKA Wanawake ambao huridhika na hali walizonazo ni kivutio kikubwa kwa wanaume. Hili ni kundi linalohitajika sana katika ulimwengu wa mapenzi kwa upande wa wanaume ambao maisha ya sasa yamekuwa yakiwageuza kutoka juu kwenda chini au chini juu. Kukubali hali zote bila kubadili tabia ni sifa njema ya mwanamke. 
 
WA MMOJA  Wanawake wanaochagua mara moja na kutosheka na kuwa tayari kukwepa kila aina ya vishawishi toka kwa wanaume ambao kimtazamo wana vitu vya ziada zaidi ya waliowachagua mwanzo, wanahitajika sana. “Niliye naye ananitosheleza kwa kila kitu sitaki mtu mwingine.” Kundi la wanawake wa aina hii ni adimu na muhimu sana."
 

Tuesday 22 April 2014

Onyo la Marekani kwa Urusi

                   Joe Biden ameonya Urusi dhidi ya kuendelea kudhibiti mji wa Crimea

Makamu wa Rais wa Marekani Joe Biden amesema sharti Urusi ikome kuongea sana na badala yake ianze kufanya kazi ya kusitisha mgogoro wa kisiasa nchini Ukraine.
Bwana Biden aliyasema hayo wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo waziri mkuu wa Ukraine Arseniy Yatsenyuk pia alihudhuria.
Marekani imeonya Urusi kuwa ikiendelea kuchochea hali nchini Ukraine , itatengwa na jamii ya kimataifa. Pia ameitaka Urusi kukomesha uungaji mkono wa vikosi vya Ukraine vinavyounga mkono Urusi.
Joe Biden, amesema kuwa Marekani iko tayari kuwasaidia viongozi wa Ukraine kufikia kile alichokitaja kuwa fursa ya kihistoria ya kujenga taifa la Ukraine lenye umoja.
Biden pia aliwahutubia wabunge mjini Kiev katika ziara iliyopangwa kuonyesha uungwaji mkono wa Marekani kwa serikali ya mpito ya Ukraine.
Bwana Biden amesema kuwa uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika mwezi ujao ni muhimu zaidi katika historia ya taifa hilo.

Wakati huohuo Biden amesema kuwa Marekani haitawai kutambua alichosema ni Udhibiti haramu wa jimbo la Crimea ambalo linadhibitiwa na Urusi. Amesisitiza kuwa Ukraine ni nchi moja na inapaswa kusalia hivyo.
Amesihi Urusi,kuhakikisha kuwa mkataba uliofikiwa wiki jana wa kusitisha mgogoro kwa kuamuru vikosi vya Ukraine vinayounga mkono Urusi nchini humo kuondoka katika majengo ya serikali waliyoyateka Mashariki mwa Ukraine.

Kadhalika Biden alisema kuwa pamoja na msaada zaidi wa dola bilioni 50 unaodhamiria kusaidia kuchepua uchumi na kuleta mageuzi ya kisiasa,Marekani pia inaahidi kutoa msaada wa kijeshi.

                           Source: BBC Swahili

David Moyes atimuliwa na Manchester United

                                Moyes amekuwa na Man U kwa miezi kumi pakee 

Mkufunzi mkuu na meneja wa klabu ya Manchester United David Moyes ametimuliwa. David Moyes amefutwa kazi baada ya kushikilia usukuni wa klabu hiyo kwa miezi kumi tu.
Klabu hiyo hapo awali ilikuwa imekataa kuzungumzia udaku wa magezti kuwa Moyes atafutwa kazi kabla ya msimu kumalizika.
Moyes, mwenye umri wa miaka 50, aliteuliwa na Ferguson kumrithi alipostaafu mwaka jana baada ya kuwa na klabu hiyo kwa miaka 26.

Taarifa kutoka kwa klabu hiyo imemshukuru Moyes kwa bidii, uaminifu na hekima aliyoonyesha kocha huyo akiwa mkufunzi wa Manchester United. Moyes alichukuwa usukani wa kuifunza Manchester United mwaka uliopita baada ya aliyekuwa kocha wa siku nyingi Sir. Alex Ferguson kustaafu.

Huku zikiwa zimesalia mechi nne pekee msimu wa ligi kukamilika Mancheseter united inashikilia nafasi ya saba kwenye jedwali la msimamo wa ligi hiyo alama ishirini na tatu nyuma ya viongozi Liverpool.
Klabu hiyo imeshindwa kufuzu kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa ulaya kwa mara ya kwanza katika kipindi cha takriban miaka ishirini

JIHADHARI NA KAULI HIZI TOKA KWA MWANAMKE

1. Mwanamke anaposema, 'sasa hivi' au 'dakika moja tu,' maana yake ni kwamba, ni nusu saa ijayo. kwa mwanamke sasa hivi ya kujiandaa ina maana sasa hivi ya muda mrefu mara sita zaidi kuliko ule
anaoutaja. kama akisema , 'nusu saa tu, naja,' unapaswa kwenda kufanya shughuli nyingine kwanza, kwa sababu huenda ukiamua kuamini kwamba ni nusu saa kweli, utasimama au kukaa mahali kumsubiri hadi miguu iingie tumboni au makalio yaote ganzi.
2. Mwanamke anaposema, 'utajua mwenyewe,' ana maana kwamba amekasirishwa na kukatishwa tamaa na tabia yako na sasa hajali tena. maana yake ni kwamba kwa upande wake haoni sababu ya kujiumiza bure na huenda atachukua uamuzi ambao nawe pia hautaufurahia. Je, anaweza kuanza kutoka nje baada ya hapo? inawezekana ingawa siyo lazima.

3. Mwanamke anapopumua kwa nguvu, yaani kushusha pumzi kwa kishindo, hiyo pia ni kauli kwa upande wake. kama anashusha pumzi kwa nguvu wakati mkijadili au kuongea jambo, ni taarifa kwamba amekudharau. yaani amekuona mjinga nambari moja. ni kauli kwamba, haoni sababu ya kuendelea kuwepo hapo kubishana nawe, kwani huna jambo la maana unalomweleza.


4. Mwanamke anaposhusha pumzi polepole, ina maana kwamba, amekubaliana na wewe. Sasa hapo usifanye kosa kwani, ukibadilika kidogo au kuleta mambo mengine kinyume na na hayo yaliyomridhisha, ndipo hapo atashusha pumzi kwa nguvu , yaani kuanza kukuona huna maana kwa wakati huo. Kumbuka kwamba, mwanamke akishusha pumzi kwa nguvu kwa maana ya kukuona huna lolote, hukuona hivyo kwa wakati ule tu au kwa hilo jambo linalohusika tu, siyo kwamba, hukuona hivyo siku au muda wote. vivyo hivyo kwenye kushusha pumzi pole pole, hukuona 'babu kubwa' kuhusiana na na jambo mnalojadili kwa wakati huo tu.

5. Mwanamke anapotumia neno, 'sawasawa,' kwa kawaida kama kuna jambo umemfanyia, ina maana kwamba, 'ninachukua muda kutafakari, halafu utaona nitakachokulipa baadaye.' Kauli hii siyo nzuri na mara nyingi ni ya hatari. Wanaume ambao wamewahi kulipiziwa visasi kwa njia mbaya na ya hatari na wapenzi wao wamekiri kuambiwa,'sawasawa,' au 'sawa bwana,' kabla ya visasi hivyo.

6. Mwanamke anapotamka neno, 'we endelea tu,' anakuwa na maana ya kwamba, siku si nyingi zijazo, atafanya jambo ambalo hutalifurahia, kama hutaacha kufanya kitu au jambo lenye kumuudhi. hiyo ni kauli ya kukutahadharisha kwamba, usije ukashangaa pale ambapo utaona amefanya kitendo cha hatari dhidi yako kutokana na tabia yako au matendo yako mabaya dhidi yake.


7. Kuna wakati mwanamke anaweza kusema, 'sawa bwana fanya,' kama kuna jambo ambalo hamjafikia muafaka au amebaini umekuwa ukifanya jambo fulani baya au lenye kumkera. Hapa hana maana kwamba, amekuruhusu kwa moyo mmoja, hapana. Hapa anataka ubaini kwamba, hajakubaliana nawe, anakupa muda wa kujaribu kutafakari tena.


8. Je kama mmeshindana katika jambo au umemkera katika jambo au mambo fulani, kutokana na tabia au mwenendo fulani, halafu akakumabia, 'asante sana,' itakuwa na maana gani? Hii ina maana umemkera kupita kiasi na bado wala hajajua akufanye nini. Hii ni toafauti na 'asante' ya kawaida. Mwanamke anapoongeza neno 'sana,'ujue umemkera hasa, kuliko unavyoweza kufikiri. Halafu kama baada ya kusema, 'asante sana,' anashusha pumzi kwa nguvu, ujue hali ni mbaya zaidi, bora unyamaze kwanza, hata radhi usiombe kwa muda huo, subiri apoe kwanza.

Msingi Muhimu kwa Familia yenye Furaha


Mwandishi maarufu wa Kirusi Leo Tolstoy alianza riwaya Anna Karenina kwa maneno haya: “Familia zenye furaha zote zinafanana; kila familia isio na furaha inakuwa haina furaha kivyake.” 1 Ingawaje mimi sina hakika ya Tolstoy kwamba furaha ya familia zote zinafanana, nimetambua kitu kimoja ambacho familia zote ni sawa sawa: zina njia ya kusamehe na kusahau upungufu wa wengine na kutafuta wema.

Wale walio katika familia zisizo na furaha, kwa upande mwingine, mara nyingi wanaona makosa, wanakuwa na kinyongo, na hawaonekani kusahau makosa yaliyopita.
“Ndio, lakini” anza na wale wasio na furaha. “Ndio, lakini haujui jinsi anavyoniumiza mimi vibaya,” asema mmoja. “Ndio, lakini haujui jinsi huyu alivyo mbaya.” asema mwingine.
 

Labda wote ni sahihi; lakini hakuna yeyote.
Kuna viwango vingi vya makosa. Kuna viwango vingi ya uchungu. Lakini kile nimeona ni kwamba kila mara tunahalalisha ghadhabu yetu na kuridhisha dhamiri zetu kwa kujiambia wenyewe hadithi kuhusu dhamira za wengine ambazo zinashutumu matendo yetu kama yasiweza kusameheka na ubinafsi, hali wakati huo huo, tukikweza dhamira zetu kama halisi na maasumu.

Mbwa wa Mwana Mfalme


Kuna hadithi ya kale ya Kiwelishi kutoka katika karne ya 13 kuhusu mwana mfalme ambaye alirudi nyumbani na kumpata mbwa wake hakitiririkwa na damu usoni mwake. Huyu mtu akakimbia ndani na, kwa kushituka, akaona kwamba mvulana mchanga wake hakuwepo na susu yake ikiwa umependuliwa. Kwa ghadhabu mwana mfalme akauchomoa upanga wake na kumuua mbwa wake. Muda mfupi baadaye, akasikia kilio cha mwanawe—mtoto alikuwa hai! Kandoni mwa mtoto mchanga alilala mbwa mwitu aliyekufa. Yule mbwa, kwa kweli, alikuwa amemlinda mtoto wa mwana mfalme kutoka kwa mbwa mwitu muuaji.

Ingawaje hii hadithi ni ya tamthiliya, inaonyesha jambo fulani. Inaonyesha uwezekano kwamba hadithi hii unatuambia kuhusu kwa nini wengine wanatenda kwa njia fulani kila mara haiambatani na sababu—ambazo wakati mwengine sisi hata hatutaki kujua sababu. Tungependa afadhali tuhisi kujihalalisha wenyewe katika ghadhabu yetu hata kwenye uchungu wetu na maudhi. Wakati mwengine hiki kinyongo kinaweza kuwa kwa miezi au miaka. Wakati mwengine kinaweza kuwa kudumu maisha.
Familia Iliyogawanyika

Baba mmoja hakuweza kumsamehe mwanawe kwa ajili ya kupotoka kutoka kwa njia aliyokuwa amemfunza. Huyu mvulana alikuwa na marafiki ambao baba yake hakupendelea, na alifanya mambo mengi kinyume na kile baba alifikiria alifaa kufanya. Haya yalileta ugomvi kati ya baba na mwana, na huyu mvulana punde alipojiweza, alihama nyumbani na asirudi kamwe.

Hawakuongeleshani tena.
Je! Huyu baba alihisi kujihalalisha? Labda
Je! Huyu mwana akihisi kujihalalisha? Labda

                                Baba, Mama na watoto
Yote ninayojua ni kwamba hii familia iligawanyika na haikuwa na furaha kwa sababu baba wala mwana hakuweza kusamehe mwenzake. Hawangeweza kuona zaidi ya kumbukumbu chungu walizokuwa nazo kuhusu kila mmoja. Walijaza mioyo yao na ghadhabu badala ya upendo na msamaha. Kila mmoja alijinyima nafasi ya kuathiri maisha ya mwenzake kwa wema. Mgawanyiko kati yao ulionekana kuwa wa kina na mpana sana kwamba kila mmoja akawa mfungwa kiroho katika kisiwa chake mwenyewe cha mhemko.

Kwa bahati nzuri, Baba yetu wa Milele aliye Mbinguni mwenye upendo na hekima alifanya njia ya kushinda ufa huu wa kiburi. Upatanisho mkuu na usio na mwisho ni tendo kuu la msamaha na suluhu. Uzito wake ni zaidi ya uelewa wangu, lakini nashuhudia kwa moyo na nafsi yangu yote juu uhalisi na uwezo wake wa msingi. Mwokozi alijitoa Mwenyewe kama fidia ya dhambi zetu. Kupitia Kwake sisi tunapata msamaha.

Friday 18 April 2014

Uamuzi uliotangazwa na Wizara ya fedha kwa UKAWA baada ya kususia vikao vya bunge la Katiba




Wizara ya Fedha kupitia Naibu wake Waziri wa fedha Mh. Mwigulu Nchemba wametangaza uamuzi wa kufuta malipo ya Wabunge waliosusia vikao vya mchakato wa Katiba vinavyoendelea Dodoma.
Uamuzi huu umetangazwa ikiwa ni siku ya pili tangu Wajumbe wa Bunge la Katiba Kutoka UKAWA wasusie Shughuli za Bunge la Katiba kwa Madai wamechoka matusi na Kuburuzwa kwenye Bunge hilo.
Hii leo Naibu waziri wa Fedha Mh.Mwigulu Nchemba ambaye kwa Sasa anakaimu Kuwa Waziri wa Fedha tangu April 10  20014 baada ya  Waziri wa Fedha kupata safari ya kikazi nchini Marekani,amefuta Malipo ya wabunge waliosusia Mchakato huo wa Katiba.
Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ameagiza Benki zote kurudisha Cheque za Malipo ya Posho na seating allowance ambazo zilipelekwa Bungeni April 16 ili ziwekwe kwenye akaunti binafsi za Wabunge ikiwa ni Malipo ya Mpaka April 30.
Uhakika wa taarifa hizi anazisema mwenyewe Mh.Mwigulu Nchemba kupitia Exclusive Interview na millardayo.com na kuelezea uamuzi huu pamoja na mtazamo wake kuhusu hili bunge la Katiba linaloendelea kwa sasa.