Thursday 30 July 2015

Afya Ni Mali



WATAFITIi wa nchini Israel walibaini kuwa, mtu anayekunywa chai mara kwa mara ana uwezo wa kuishi muda mrefu tofauti na yule asiyependa chai.


Aghalabu maisha ya mwanadamu yeyote yule yapo mikononi mwa muumba wake, ambaye hujua lini muda wa kuishi wa kiumbe wake utakwisha. Lakini mtindo wa maisha yetu usiojali kanuni za afya, umeonyesha kuwa ndicho chanzo cha watu wengi kuishi maisha mafupi.


Kiwango cha maisha ya binadamu sasa kinapunguzwa kutokana na mabadiliko ya tabianchi, mtindo wa maisha na mazingira, lakini wanasayansi na wataalamu wa afya wamekuja na mbinu ambazo zinatajwa kusaidia kuongeza miaka yako ya kuishi.

KUNYWA CHAI Watafiti wa nchini Israel walibaini kuwa, mtu anayekunywa chai mara kwa mara ana uwezo wa kuishi muda mrefu tofauti na yule asiyependa chai.

Chai, hasa ya kijani (green tea) ina ondoa sumu iitwayo ‘polyphenols’ ambayo husaidia mwili wako kupambana na magonjwa ya moyo. Wataalamu hao wanasema, chai iliyochemka vizuri au pakiti ya majani ya chai kukorogwa vyema katika majimoto, yafaa zaidi. Kwa kifupi, chai ikolee majani.

KUSIMAMA KWA MGUU MMOJA KILA ASUBUHI Inaweza kuonekana kuwa ni jambo la ajabu, lakini wanasayansi wamebaini kuwa kusimama kwa mguu mmoja asubuhi kunasaidia kuimarisha misuli ya mgongo, nyonga na tumbo na kuupa uwiano uti wa mgongo.



Mtaalamu wa viungo anasema, zoezi hili jepesi likifanywa kila siku, linatoa manufaa ya muda mrefu na linakukinga kuvunjika mifupa kwa urahisi hasa unapoanza kuzeeka. Tafuta marafiki sita unaowaamini Kuwa na marafiki wazuri na familia ambayo unaiamini ni siri moja kubwa ya kuishi miaka 100.

Utafiti uliofanywa na kitengo cha Maisha na Mazingira katika Chuo Kikuu cha Australia, ulionyesha kuwa kupata watu wa kukupa msaada na kukufariji wakati wa huzuni kunasaidia kuongeza umri wa kuishi kwa kuzalisha kemikali ya ‘furaha’ inayofahamika kama dopamine na oxtocyin ambavyo huusaidia ubongo.

Mwanasaikolojia wa Chuo Kikuu cha Dodoma, anasema unapokuwa na tatizo, kisha ukalihifadhi moyoni, unaunda uchungu ambao unakuathiri. Anasema, mwili wa mtu unaathiriwa kutokana na tabia au matendo ya moyoni, unapohifadhi tatizo bila kupata ushauri unakuza tatizo hilo.“Marafiki au hata ndugu wa kumweleza tatizo lako ni muhimu, wanaweza kukupoza,” anasema


USISHIBE SANA Wakazi wa kisiwa cha Okinawa, nchini Japan, wanaongoza kwa kuwa na kiasi kidogo cha watu wenye unene uliopitiliza (obesity) na wanasifika kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaoishi zaidi ya miaka 100. Siri yao kubwa ni kuwa hawali wakashiba kwa zaidi ya asilimia 80.


Watafiti wa Marekani pia, wamebaini kuwa, binadamu wanaweza kuishi miaka mingi zaidi iwapo chakula wanachokula kinapunguzwa kwa robo tatu. Ina maana kwamba kula kidogo kunaufanya mwili wako usiwe na kazi kubwa ya kumeng’enya, hivyo kuupa nafasi ya kuwajibika na kazi nyingine.

Mtaalamu wa chakula na lishe, anasema, mtu hatakiwi kula akashiba bali anatakiwa aache njaa kwa mbali ili kutoa nafasi ya maji na mmengenyo kuchukua nafasi.

LALA KWA MUDA MREFU Ukosefu wa usingizi unakuweka katika hatari kubwa ya kupata maradhi ya msongo wa mawazo na moyo. Kupata makunyanzi na mwili kuchoka.



Mabadiliko kidogo tu ya kitabia yanaweza kuleta mapinduzi makubwa katika afya yako. Wanaopata usingizi wa kutosha si rahisi kupatwa na kiharusi au shinikizo la damu.

PIGA MSWAKI
Maradhi ya fizi, ni maradhi yaliyopata umaarufu duniani. Dk James Russel wa kituo cha tiba cha Hope, anasema, meno na fizi ni chanzo cha magonjwa mengi ambayo wengi hudhani hayahusiani na afya ya kinywa. Maradhi ya fizi yanatajwa kuwa chanzo cha saratani za aina fulani, maradhi ya moyo, ubongo na hata kisukari.


KUWA MAKINI

Utafiti uliofanywa na Mwanasaikolojia wa nchini Marekani, Dk Howard Friedman unasema kuwa, umakini wa mtu ni kigezo cha urefu wa maisha yake. Watu ambao wapo makini na maamuzi, matumizi ya fedha na ambao wanapenda kuweka kila kitu sawa na kufanya mambo yao kwa uangalifu, wanaweza kuishi kwa muda mrefu.


KWA NINI? Dk Kitila Mkumbo, Mwanasaikolojia wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE) anasema, unapokuwa makini unafanya uamuzi mzuri ambayo hupunguza kiwango cha kuishi maisha hatarishi.


“Umakini unamsaidia mtu kuepuka tabia hatarishi kwa mfano ngono zembe, kuvuta sigara, mambo ambayo yanahatarisha afya,” anasema.

Anasema, mtu anayepangilia mambo yake na kuwa makini kwa mfano kutumia kinga wakati wa tendo la ndoa kunakuepusha na maambukizi ya maradhi mbalimbali.

USIWEKE MATUNDA KWENYE JOKOFU Unaweza kufikiri kuwa, kuyaweka matunda katika jokofu, unayafanya yadumu kwa muda mrefu, lakini tafiti zinaonyesha kuwa, matunda yaliyopoozwa kwa baridi ya jokofu, yanapungukiwa vitamini muhimu kuliko matunda yanayowekwa katika hali ya kawaida.


Kwa mfano, nyanya na pilili ni vyema kuwekwa katika bakuli kuliko katika jokofu. Matunda mengi yanasaidia kuondoa sumu mwilini hivyo lishe zake zikibaki bila kuharibiwa, husaidia kujenga moyo imara na kupunguza kiwango aina fulani za saratani.


KUFANYA TENDO LA NDOA ANGALAU MARA MBILI KWA WIKI
Utafiti mkubwa na uliothibitishwa wa Welsh na wenzake wa Hospitali ya Royal Edinburgh, Uingereza ulibaini kuwa wale wanaofanya mapenzi mara moja kwa mwezi wapo katika hatari ya kufa mapema, ukilinganisha na wale wanaofanya mapenzi mara mbili kwa wiki.



Welsh anasema, tendo la ndoa linapunguza msongo wa mawazo na kumfanya mtu apate usingizi mzuri. Msongo wa mawazo unasababisha maradhi ya moyo na kisukari. Dk Mkumbo anasema, tendo la ndoa ni jambo la afya na husaidia katika kupunguza msongo wa mawazo na kuupa mwili uchangamfu. Hata hivyo Dk Mkumbo anasema hajawahi kusikia idadi ya siku za kufanya mapenzi kama ni mara moja au mbili kwa wiki, bali anaamini kitendo chenyewe kina umuhimu wake kiafya.


Kwa nini Wajapan wanaishi maisha marefu? Inaelezwa kuwa Wajapan ni taifa linaloongoza kwa kuwa na watu wanaoishi muda mrefu kuliko mataifa mengine. Takwimu za Shirika la Afya Duniani zinaeleza kuwa, raia wa Japan wanaishi maisha marefu zaidi. Kwa mfano, mwanaume mzee kuliko wote aliyevunja rekodi ni Jiroemon Kimura, kutoka Kyotango, Kyotto, Japan aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 116. Siri yao kubwa ni kula chakula chenye afya ikiwemo samaki badala ya nyama nyekundu.



Hawanywi maziwa, au bidhaa zozote za ng’ombe. Nafaka jamii ya soya ambazo zinasaidia kuondoa maradhi ya moyo. Wanakunywa chai kwa wingi, hasa ya kijani, wanakula kiasi kidogo cha chakula, hawatumii magari mara kwa mara na wanatumia vyoo vya kuchuchumaa badala ya vya kukaa.



..inaonekana hizi TAFITI zinashabiana na WATAFITIi wa hapa nchini na nje waliobaini haya:-

wataalamu na wanasayansi nchini wametaja mbinu mbalimbali ambazo binadamu akizifuata, anaweza kuishi zaidi ya miaka 100. Wataalamu hao, kutoka vitengo mbalimbali vya Sayansi ya Jamii na Viumbe hapa nchini, wamesema mtu akiishi bila kuathirika akili na mwili, anaweza kuishi maisha marefu zaidi kuliko yule anayeathirika katika vitu hivyo. Wasomi hao wamebainisha kuwa mgawanyo wa mwili, akili na roho, ni mambo muhimu katika mwili wa mwanadamu yaliyo na uwiano unaoingiliana na havitenganishik i.

Kukabili msongo wa mawazo
Akizungumza na Mwananchi Jumapili, Mtaalamu wa Saikolojia na Mkuu wa Kitengo cha Sosholojia wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Joyce Nyoni aliitaja mbinu ya kwanza ya kuongeza maisha kuwa ni kukabiliana na msongo wa mawazo. Daktari huyo alisema akili ya mtu huweza kuathiri mwili. Wengi wamekuwa wakipoteza maisha kutokana na maradhi yanayotokana na msongo wa mawazo, kama vile maradhi ya moyo au vidonda vya tumbo. “Wengi wetu tuna msongo wa mawazo, jambo dogo linaweza kumfanya mtu akashindwa hata kula au kulala, ni lazima tujifunze kukubaliana na hali halisi ya maisha, huku tukiamini kuwa, hakuna jambo lisilo na utatuzi,” alisema Dk Nyoni.

Alisema wapo wanawake wengine ambao hupoteza maisha kwa sababu ya waume zao kuwatesa au kuwatelekeza. “Ni lazima tufahamu kuwa maisha hata siku moja hayawezi kunyooka, ni lazima viwepo vikwazo vya hapa na pale, kwa hiyo hatuna budi kujifunza kuzikabili changamoto za maisha,” alisema. Utafiti uliwahi kufanyika na kuonyesha kuwa, wanawake chini ya miaka 50 na walio katika kipindi cha kufunga hedhi, (menopause) ambao hawawezi kukabiliana na msongo wa mawazo, wanaugua maradhi ya moyo. Alisema yeye kama mtaalamu wa masuala ya saikolojia, huwashauri watu kutulia na kukubaliana na matokeo yoyote katika maisha.


Kuishi mfumo chanya, kucheka
Jambo lingine ambalo mtaalamu huyu alishauri ni kuishi katika mfumo chanya. Alisema watu wengi hawatosheki na kile kidogo wanachopata, badala yake wanaishi kwa kulalama jambo ambalo kwa asilimia kubwa, huchangia maradhi ya moyo. “Mara kwa mara huwa nawaeleza wanafunzi wangu, ukimwona mwanamke kavaa mikufu, bangili na hereni nyingi masikioni, vyote vya dhahabu, huyo ni mgonjwa, kwa sababu ukimnyang’anya au akiibiwa ujue ataugua,” alisema Dk Nyoni. Alisema, ni vyema watu waishi kwa kuridhika na chochote wapatacho, badala ya kutoridhika na hali yao na kutamani maisha ya wengine.

“Namthamini mwanamke anayetoka nyumbani, amechana nywele zake kawaida, amepaka mafuta, lakini anajiamini, kuliko yule ambaye anataka atazamike kuwa ni wa thamani na mwenye fedha, mbele za watu, kwa kuvaa nguo za thamani kubwa au kuendesha magari ya kifahari,” alisema .Mtaalamu huyo alitaja mbinu nyingine ya kurefusha maisha kuwa ni kucheka au kuwa na furaha

Mazoezi, usingizi wa kutosha

Naye Dk Nandera Mhando, wa Kitengo cha Sosholojia na Athropolojia cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alisema hakuna ubishi kuwa zipo tabia ambazo husababisha baadhi ya watu kukumbwa na maradhi na kufa katika umri mdogo. “Wapo ambao hawana kabisa tabia za kufanya mazoezi, hawa huwa na uzito mkubwa na miili yao inapokuwa na mafuta mengi, maradhi ya moyo huwa yamepata nyumba, lakini pia kutopata usingizi wa kutosha nalo ni tatizo,” alisema.

Tabia ya mtu, vyakula

Dk Mhando alisema, tabia ya mtu ni sababu nyingine inayoweza kumfanya mtu awe na maisha mafupi, kwa mfano, kupenda kufanya ngono, kuvuta sigara, na ulevi ni mambo yanayosababisha maradhi na kuleta kifo.

“Kama mtu tayari ameathirika, halafu anandelea kufanya ngono kwa kiasi kikubwa, si ajabu mtu huyo kufa mapema, lakini wanaokunywa pombe na kuvuta sigara kwa wingi, nao mara nyingi huugua maradhi ya figo, mapafu, ini nk.,” alisema. Daktari huyu aliongeza kwamba, aina za vyakula tunavyokula nayo vinachangia kupima afya ambayo kimsingi ni kipimo cha maisha ya binadamu.

Alisema wanaokula vyakula asilia, kama mboga za majani, kunywa maji na kula matunda kwa wingi, si rahisi kushambuliwa na maradhi, tofauti na wanaokula wanga peke yake ambao wanakuwa katika hatari ya kupata maradhi, hatimaye kifo. Imethibitishwa kuwa, Mwanabaolojia mmoja, wa nchini Marekani, Ancel Keys, hata baada ya kustaafu, aliendelea kufanya kazi za bustani nyumbani kwake kwa kiasi kikubwa jambo lililomfanya kuishi miaka 100. Alifariki mwaka 2004.

Dini
Mtaalamu wa Sosholojia ya Dini kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Thomas Mwendaluka, alisema, dini ni moja ya maeneo ambayo huweza kuchangia mtu kuishi maisha marefu.


“Dini ina pande mbili, hasi na chanya, kwa sababu kwa upande mmoja inatoa tumaini. Inamsaidia mtu kiimani kuishi maisha marefu na vilevile ni chanzo cha kufupisha maisha,” alisema Mwendaluka. Alisema, watu huweza kujengwa kiroho na kuamini uponyaji wa magonjwa yaliyoshindikan a. Kwa mfano tangu UKIMWI ulipoingia , waathirika wengi wamekimbilia katika taasisi za dini na kule hujengwa kiroho na kiimani na kujisikia wamepona na kuongeza siku za kuishi. “Lakini baadhi ya imani, kwa mfano Boko Haram, zinawataka waumini wajitoe muhanga kuua, hilo hufupisha maisha ya wengi,” alisema Mwendaluka. David Larson, Mshauri wa Taasisi ya Taifa ya Afya ya Akili wa nchini Marekani, alifanya utafiti wake mpana juu ya uhusiano wa moja kwa moja uliopo kati ya dini na afya.

Uchunguzi wake ulionyesha wazi kwamba upo uhusiano wa moja kwa moja kati ya muumini aliyejitoa kwa moyo katika imani husika na afya yake. Alishangaa kubaini kwamba, wale wanaohudhuria kanisani wanaishi muda mrefu kuliko wale wasiohudhuria. “Nilishangazwa kujua kuwa kutumainia uweza wa Mungu ndio msingi wa ustawi wa kweli na maisha ya afya yenye furaha,” alisema Larson.

Kunywa maji mengi


Daktari wa Kitengo cha Patholojia katika Hospitali ya Muhimbili, Innocent Mosha anasema maji ni jambo lingine linaloweza kukupa afya na kukuepusha na maradhi. “Kazi ya maji ni kusafisha ini na figo, kwa hiyo si ajabu mtu asiyekunywa maji ya kutosha akawa na afya mbaya kwa sababu uchafu hubaki katika damu,” alisema Dk Mosha. Matabibu wengi wanashauri kuachana na aina za vyakula kwa mfano, nyama ya wanyama yenye mafuta ya majimaji (saturated fat) na mafuta mazito (cholesterol), ambavyo huongeza hatari ya kupata shinikizo la damu, kupooza

(stroke), ugonjwa wa moyo, kansa, unene usio wa kawaida, kisukari na magonjwa mengineyo. Mwandishi wa kitabu cha ‘The Blue Zones’ Dan Buettner, ambaye alifanya utafiti kuhusu siri ya ya kuishi maisha marefu katika nchi za Bara la Australia, Greece na China, aligundua kuwa, watu wa nchi hizo wana tabia za kufanana ambazo bila shaka huwafanya waishi maisha marefu. Alisema wote hula milo yenye kiasi kidogo cha nyama na wanafanya mazoezi.


=============
1. Jiweke mbali na sigara.
2. Epuka unene.
3. Fanya mazoezi.
4. Kula lishe bora.
5. Hakikisha unacheki na kupima kiwango cha kolestero mwilini, shinikizo la damu na sukari na kuhakikisha viko katika kiwango kinachotakiwa.
Uchunguzi huo umeonyesha kwamba watu wengi umri wa kuanzia miaka 50 ambao wanaishi kwa kufuata masharti hayo huwa na uwezo wa kuishi miaka 40 zaidi bila kupata shinikizo la damu na ugonjwa wa moyo, ambayo ni magonjwa makuu mawili yanayoua watu zaidi duniani. Wataalamu wamesema kwamba, kila mtu anayetaka kuishia maisha marefu anatakiwa kufuata ushauri ufuatao:
• Jiepushe kuvuta sigara au acha kuvuta sigara kabisa.
• Kila wiki pata dakika zisizopungua 150 za kufanya mazoezi ya kawaida.
• Jitahidi kufuata maelekezo ya kula lishe bora ambayo ni: vikombe 4 na nusu vya matunda na mboga mboga kwa siku, samaki mara mbili au tatu kwa wiki. Usinywe sana vinywaji vyenye sukari, kula vyakula vyenye ufumwele kila siku na chumvi isizidi miligram 1,500 kwa siku.

• Kiwango cha kolestero au mafuta katika damu yako kisizidi 200.
• Shinikizo lako la damu lisiwe zaidi ya 120 chini ya 80.
• Sukari katika damu iwe chini ya 100


Source: Jamiiforums Apr 17, 2014

"ULIYENAE ANAKUPENDA KWA DHATI"..

                     Chistopher Peter katika njia mojawapo ya ushiriki wa matukio ya kijamii. Safari ya maisha kama vijana ni ndefu sana katika kufikia malengo.

"Kijana Zamu Yako Sasa 2015 nenda kajiandikishe" 

NUSU FAINALI KAGAME KIINGILIO BUKU TATU TU

          Kikosi cha Azam FC
Hatua ya nusu Fainali ya Michuano ya Kombe la Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup) inatarajiwa kuendelea kesho katika uwanja wa Taifa, huku kiingilio cha chini katika michezo hiyo kikiwa ni shilingi elfu tatu (3,000).
Viingilio vingine vya michezo hiyo ya kesho  ni VIP A ni shilingi elfu kuni na tano (15,000) na VIP B & C, Shilingi elfu kumi (10,000) na sehemu nyingine ya uwanja  iliyobakia ni shilingi elfu tatu (3,000) kwa viti vya rangi ya bluu, kijani na rangi ya chungwa.
Timu nne kutoka katika nchi nne wanachama wa michuano hiyo, Azam FC (Tanzania), Gor Mahia (Kenya), KCCA (Uganda) na Al Khartoum (Sudan) zimefuzu kwa hatua ya nusu fainali itayochezwa uwanja wa Taifa siku ya ijumaa.


Mchezo wa kwanza utakaonza saa 7:30 mchana utazikutanisha timu za Gor Mahia ya Kenya itakayocheza dhidi ya Khartoum ya Sudan, mchezo unaotarajiwa kuwa wa vuta nikuvute kufutia timu hizo kutoka sare katika mchezo wake wa awali hatua ya makundi.
Katika mchezo wa kwanza uliozikutanisha timu hizo, kocha wa Khartoum Kwesi Appiah na Frank Nuttal wa Gor Mahia walitoka sare ya bao 1- 1 ndani ya dakika 90, hali ambayo inapelekea kufaya mchezow wa kesho kuwa mgumu kwa kila timu kuhitaji nafasi ya kusonga mbele hatua ya fainali.
Gor Mahia mabingwa mara tano wa michuano hiyo, wataingia uwanjani kusaka ushindi ili kusonga hatua ya fainali ili waweza kutwaa ubingwa huo kwa mara ya sita, sawa na klabu ya Simba inayoongoza kwa kutwaa ubingwa huo.

Kocha Frank Nutta atakua akiwategemea wachezaji wake nyota, Khalid Alucho, Kagere Meddie, Michael Olunga, Sibomana Abouba, Karim Nzigiyimana, Godfrey Walusimbi, Nahodha Musa Mohamed, na mlinda mlango Boniface Oluoch katika kusaka ushindi dhidi ya Khartoum.
Kwesi Appiah atashuka dimbani akiwategemea wachezaji wake nyota, Antony Akumu, Dominic Abdui, Samawal Meshani, Wagdi Wawd, Ouismaila Baba na nahodha Amin Ibrahim.
Vita kali itakua kwa washambulaji Michael Olunga wa Gor Mahia na Salaheldin Osman wote wenye mabao manne, wakiwania kuongeza bao katika mchezo huo wa kesho ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa kiatu cha dhahabu.

Nusu fainali ya pili itawakutanisha waoka mikate wa Azam FC dhidi  ya Mamlaka ya jiji la Kampala (KCCA), mchezo utaokanza majira ya 9:30 kwa saa za Afrika na Kati katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mchezo huo pia unatarajiwa kuwa na upinzani mkali kufutia timu hizo katika mchezo wa hatua ya makundi, Azam FC kuibuka na ushindi wa bao 1- 0, bao liliofungwa na nahodha wake John Bocco.
KCCA chini ya kocha wake Mike Mutebi watashuka dimbani kusaka ushindi katika mchezo huo, ikiwa ni kulipiza kisasi kwa mchezo wa kwanza na kupata ushindi utakaowavusha mpaka katika hatua ya fainali.

Kocha Mutebi atakuwa akiwategmea wachezaji wake nyota, Nahodha Tom Matiko, Opio Emmanuel, Joseph Ochaya, Hassan Waswa, Isaac Sserenkuma, Habib Kavuma na Muzamil Mutyaba.
Azam FC itashuka dimbani kutaka kuendeleza ubabe wake dhidi ya KCCA ya Uganda, na kuweza kukata tiketi ya kucheza fainali siku ya jumapili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kocha wa Stewart Hall wa Azam atakua akijia safu yake ya ulinzi ambayo haijaruhusu bao tangu kuanza kwa michuano hiyo, huku safu yake ya ushambuliaji ikiwa imefunga mabao 8 katika michezo mine iliyocheza.
Hall atashuka dimbani akiwategema nyota wake Nahodha John Bocco, Pascal Wawa, Aggrey Morris, Himid Mao, Kipre Tchetche, Jean Baptist Mugiranenza, Frank Domayo na mlinda mlango Aishi Manula.

TFF YAIPONGEZA AZAM FC
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi ametuma salam za pongezi kwa klabu ya Azam FC kwa kufanikiwa kuingia katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Kagame inayotimua vumbi jijini Dar es salam.
Katika salamu zake kwa uongozi wa klabu ya Azam, Malinzi amewataka kutobweteka na kuongeza bidii katika hatua hiyo ya nusu fainali ili waweze kufuzu kwa hatua ya fainali na kutwaa Ubingwa huo na kuwaomba watanzania wote kuwasapoti wawakilishi pekee wa nchi kwenye michuano hiyo
TFF kwa niaba ya familia ya mpira na watanzania wote, inatwakia kila la kheri Azam FC katika mchezo wake wa kesho wa nusu fainali dhidi ya KCCA.

TFF YATUMA SALAM ZA RAMBIRAMBI

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limetuma salam za rambi rambi kwa familia ya Moshi Shaban, kufutia kifo cha Moshi kilichotokea jana jijini Dar s salaam na mazishi kufanyika leo jijini Dar es salaam.

 Katika salamu zake za rambirambi kwa familia ya marehemu Moshi, TFF imewapa pole wafiwa, ndugu jamaa na marafiki na kusema wako pamoja katika kipindi hiki cha maombelezo na kuomba mwenyezi Mungu awajilie nguzu wafiwa


Marehemu Moshi Shaban ni baba wa wachezaji waliowahi kuichezea timu ya Taifa ya Tanzania, Haruna Moshi “Boban) na Iddy Moshi (Mnyamwezi).

HII SIMBA NOMA!

SIMBA ilitaka kushiriki Kombe la Kagame la mwaka huu, lakini Yanga ikaanzisha chokochoko ikitishia kujitoa kama Mnyama angeingizwa.
Lengo la Jangwani lilikuwa kuhakikisha inafikia rekodi ya wapinzani wao hao ya kutwaa mara nyingi mataji ya michuano hiyo.
Simba ndiyo mabingwa wa kihistoria wakiwa wamenyakua mataji sita tangu michuano hiyo ilipoanzishwa mwaka 1974 wakati Yanga imefanya hivyo mara tano sawa na Gor Mahia, AFC Leopards na Tusker zote za Kenya.
Hata hivyo hali haikuwa kama ilivyotarajiwa jana Jumatano kwani mastraika wake nyota; Amissi Tambwe, Donald Ngoma na Geofrey Mwashiuya walishindwa kufurukuta mbele ya Azam na timu hiyo kutolewa katika robo fainali kwa mikwaju ya penalti 5-3.
Yanga ilikwama katika pambano hilo lililochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam baada ya kumaliza dakika 90 huku ikibanwa kila kona.

Kikosi cha Simba SC
Baada ya mwamuzi, Davies Omweno, kuamuru mikwaju hiyo ndipo Yanga ikajikuta ikipoteza penalti moja iliyopigwa kidhaifu na beki wake, Mwinyi Haji.
Azam ilipata penalti zake kupitia Kipre Tchetche, John Bocco, Himid Mao, Sergie Wawa na Aggrey Morris, huku Salum Telela, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Geofrey Mwashiuya wakifunga kwa upande wa Yanga ambayo haikupiga penalti ya mwisho.
Azam iliyoungwa mkono na mashabiki lukuki wa Simba, ilionyesha dhamira ya kusonga mbele kwa kuibana Yanga karibu muda wote wa mchezo.
Mabeki wa kati wa Azam Aggrey Morris na Sergie Wawa walimdhibiti vilivyo straika mpya wa Yanga, Donald Ngoma kiasi cha kutokuwa na makeke katika muda wote.
Kwenye penalti Mwinyi alizamisha jahazi la Yanga kwa mkwaju wake kudakwa na kipa Aishi Manula na safari ya Yanga kumalizikia hapo.
Kwa ushindi huo Azam itakwaana na KCCA kesho Ijumaa katika nusu fainali baada ya Waganda hao kushinda mapema jana mchana dhidi ya Al Shandy kwa mabao 3-0.
Mabao ya KCCA katika mechi hiyo yalitumbukizwa wavuni na Ochaya Joseph, Matovu Farouq na Tom Masiko. Azam itakutana na KCCA ikiwa ni mara ya pili, kwani zote zilikuwa kundi moja na katika mchezo wao Waganda walikubali kipigo cha bao 1-0. Nusu fainali nyingine itakayopigwa kesho itazikutanisha Gor Mahia ya Kenya inayopewa nafasi kubwa ya kufikia rekodi ya Simba ya kutwaa mataji sita itakayovaana na Al Khartoumn ya Sudan ambayo iliifurusha APR ya Rwanda 4-0 juzi.

Yanga imekatwa



https://encrypted-tbn3.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcQbUuTEj9npUbzem_59rcZtLFA4-SAVEIKryq-XNDzQ3JvWoDiR

Beki wa Yanga, Juma Adbul (Kushoto) akimzuia winga wa Azam, Farid Mussa wakati wa mechi ya robo fainali ya mashindano ya Kombe la Kagame iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Azam ilishinda kwa penalti 5-3. Picha na Said Khamis. 
Kwa ufupi
Yanga imetolewa kwenye michuano ya Kombe la Kagame na timu ya Azam kwa mikwaju 5-3 ya penati.
Dar es Salaam. Azam imezima ndoto ya Yanga ya kutwaa taji la sita la mashindano ya Kombe la Kagame baada ya kuitoa kwa penalti 5-3 katika  mchezo wa robo fainali uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Baada ya timu hizo kumaliza dakika 90, bila ya kufungana ndipo ilipokuja changamoto ya mikwaju ya penalti ambayo mwaka huu imekuwa mwiba mchungu kwa Yanga ambayo kabla ya penalti za jana tayari ilishakosa penalti tatu katika michezo ya hatua za makundi.
Shujaa wa Azam katika mchezo wa jana alikuwa ni kipa Aishi Manula aliyechaguliwa mchezaji bora wa mechi baada ya kudaka penalti ya tatu ya Yanga iliyopigwa na Haji Mwinyi.
Azam iliyoanza kupiga penalti ilipata penalti zake zote tano zilizopigwa na Kipre Tchetche, John Bocco, Himid Mao, Pascal  Wawa na Aggrey Morris wakati kwa upande wa Yanga waliopata ni Salum  Telela, Nadir Haroub na Godfrey Mwashiuya huku Mwinyi akikosa.
Akizungumzia mchezo huo kocha wa Yanga, Hans Pluijm alisema ameumia kupoteza mchezo huo ambao kwake ulikuwa kama fainali.
“Kupoteza mchezo huu ni pigo kwangu, kwa sababu tulikuwa na malengo ya kutwaa ubingwa katika ardhi ya nyumbani.”
Pluijm alisema,“Kipindi cha kwanza hatukucheza vizuri, japo kipindi cha pili tulitengeneza nafasi nyingi zaidi, lakini mashuti yetu mengi hayakulenga goli.
“Sasa nguvu zetu tunaelekeza katika maandalizi yetu ya ligi inayokaribia kuanza hivi karibuni,” alisema Mdachi huyo.
Kwa ushindi huo sasa Azam itacheza nusu fainali Ijumaa na KCCA ukiwa kama marudiano ya mchezo wa Kundi C ambao Azam walishinda 1-0.
Katika mchezo wa jana timu hizo zilianza mchezo kwa kasi na kushambulia mfulululizo tangu dakika ya kwanza ambapo Azam ilikosa bao baada ya krosi ya Shomari Kapombe kuwapita mabeki wa Yanga, lakini John Bocco alishindwa kufunga.
Yanga ilijibu mapigo dakika moja baadaye kupitia mshambuliaji wake Donald Ngoma aliyewatoka mabeki wa Azam na kupiga shuti lililopanguliwa na kipa  Aishi Manula na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda.
Kipa wa Azam, Manula alilazimika kufanya kazi ya kupangua shuti la Juma Abdul alililopiga akiwa umbali wa mita 18 katika dakika ya 8.  Pia mpira wa kurushwa wa Mbuyu Twite nusuru uingie golini kama si ustadi wa Manula kuutoa nje. 
Yanga iliyokuwa ikitumia mfumo wa 4-2-3-1 ambao ni mabeki wanne wakisaidiwa na viungo wawili wakabaji, viungo watatu washambuliaji na mshambuliaji mmoja, ilifanya mashambulizi mengi kipindi cha pili.
Azam iliyokuwa ikitumia mfumo wa 4-3-3, ambao ilitumia mabeki wanne, viungo watatu na washambuliaji watatu, ilitumia mashambulizi  ya kushtukiza na katika dakika 34 nusura ipate bao, lakini shuti la Tchetche lilipanguliwa na kipa wa Yanga, Mustapha ‘Barthez’ na kurudi uwanjani na kumkuta Himid Mao aliyepiga shuti la chini na Tchetche alipojaribu kuunganisha mpira ulipaa juu.
Tofauti na michezo iliyopita, jana washambuliaji wa Yanga, Tambwe,  Ngoma, Mwashiuya na Kaseke walikuwa kwenye wakati ngumu mbele ya ngome ya Azam iliyoongozwa na Wawa, Morris, Kapombe na Kheri  Abdallah iliyocheza kwa maelewano makubwa kuziba njia.
Kipindi cha pili kocha wa Azam, Stewart Hall aliwapumzisha Frank Domayo, na Kheri Abdallah na kuwaingiza Ame Ally na Said Morad wakati Hans Pluijm aliwatoa Kaseke, Juma Abdul, Niyonzima na kuwaingiza Salum Telela, Joseph Zutah na Malimi Busugu.
Pamoja na mabadiliko hayo bado timu hizo ziliendelea kutengeneza nafasi nyingi za kufunga, lakini hakuna timu iliyofanikiwa kutumia na mchezo ukaingia katika ubabe wa hapa na pale.
Twite alinusurika kupewa kadi nyekundu katika dakika ya 74 baada ya kumchezea vibaya Himid Mao wakati akiwa tayari na kadi ya njano aliyopewa dakika 71 kwa kumchezea vibaya Mao. Pia Jean-Baptiste Mugiraneza alipewa kadi ya njano kwa kumchezea vibaya Tambwe dakika 78.
Hadi filimbi ya mwisho inapigwa kuashiria kumalizika kwa mechi hiyo, Azam ilikuwa imetunza rekodi yake ya kutofungwa bao lolote hadi sasa katika mashindano hayo, wakati Yanga ikiwa imefungwa mabao mawili.
Awali KCCA ya Uganda ilijihakikishia kucheza nusu fainali baada ya kuichapa Al Shandy ya Sudan kwa mabao 3-0 kwenye Uwanja huo.
Mabao ya Joseph Ochaya, Muzamir Mutyaba na Tom Masiko yalitosha kuihakikishia KCCA kufuzu kwa nusu fainali kwa mara ya pili mfulululizo.
 Mabingwa hao wa 1978 ni mara ya kwanza katika mashindano ya mwaka huu kufanikiwa kufunga mabao matatu kwani katika mechi zake tatu zilizopita ilifunga mabao mawili tu

Wednesday 29 July 2015

REKODI INAWABEABA YANGA, KAGAME INAWAPA AZAM USHINDI.



Wachezaji Ame Ally, Kipre Tchetche na John Bocco wanataraji kuanza katika safu ya mashambulizi ya Azam FC wakati itakapo wavaa Yanga SC katika mchezo wa Robo fainali ya michuano inayoendelea ya Cecafa Kagame Cup 2015.

Timu hizo bora zaidi katika soka Tanzania Bara zitakutana kwa mara ya pili katika michuano hiyo. Mara ya mwisho zilikutana katika mchezo wa Fainali miaka mitatu iliyopita na Yanha walishinda kwa mabao 2-0 katika mchezo wa fainali na kutwaa ubingwa wao wa Tano. MECHI YA LEO..... Azam FC haijaruhusu goli lolote huku ikiwa imeshinda michezo yote mitatu iliyopita na kufunga mabao Tisa, wakati wapinzani wao Yanha wanaingia katika mchezo wa leo wakitoka kushinda michezo mitatu ,mfululizo.
Yanga imepoteza mchezo mmoja kati ya minne iliyokwisha cheza katika hatua ya makundi. Ikiwa imetoka kundi gumu zaidi katika michuano ya mwaka huu, mabingwa hao mara mbili mfululizo wa zamani wangependa kuungana na Al Khartoom na Gor Mahia ambazo tayari zimefuzu kwa nusu fainali.

Timu hizo za Sudan Kaskazini na Kenya zilikuwa kundi A pamoja na Yanga. BOCCO, AME & KIPRE Walinzi wa Yanga watakutana na washambuaji wa ' daraja la juu Afrika Mashariki na Kati'.
Kipre tayari amefunga mabao Matatu katika gemu tatu zilizopita, wakati Bocco amefunga mara mbili. Nyota hao wawili wamekuwa wakiifunga Yanga mara kwa mara na wanaweza kufanya hivyo kwa mara nyingine Jumatano hii na kuipeleka timu yao nusu fainali. Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub na ' patna wake' Kelvin Yondan walionekana kupata shida sana wakati walipokutana na GOR ambayo ilikuwa ikipanga na kufanya mashambulizi ya uhakika siku ya ufunguzi na walionekana ' kuteswa-kimtindo' na kinara wa mabao katika michuano hii, nahodha wa Al Khartoum, Salh Eldin katika mchezo wa mwisho wa hatua ya makundi ambao walishinda 1-0.
Joseph Zuttah na Mwinyi Hajji wamecheza vizuri hadi sasa, walinzi haoo wa pembeni-Kulia na Kushoto watalazimika kucheza vizuri zaidi wakati watakapoikabili safu ya mashambulizi ya Azam FC.
 Zuttah amekuwa akipandisha timu kwa mashambulizi ya uhakika akitokea upande wa kulia, Wakati Mwinyi amekuwa imara, mwepesi na mwenye pasi za uhakika katika beki mbili. Wawili hao ambao wamechukua nafasi za Juma Abdul na Oscar Joshua wameifanya safu ya ulinzi wa kati kuwa na utulivu.
Yanga watashambulia kama kawaida yao na watatumia zaidi sehemu za pembeni ili kufikisha mipira mbele kwa k uwa eneo la katikati ya uwanja linataraji kuwa ' gumu' kupitisha mipira kutokana na aina ya wachezaji ambao watacheza sehemu hiyo.
Jean Mugiraneza, Salum Abubakary na Himid Mao wanaweza kuanzishwa kama viungo watatu wa Azam FC, wakati, Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima na Deus Kaseke wanaweza kuanza katika nafasi ya kiungo upande wa Yanga.
 Azam wamekuwa wakitumia nguvu zaidi katika idara nyingi lakini wachezaji wao wa nafasi ya kiungo ni wagumu huku pia wakiwa na ufundi wa kumiliki mpira.
Niyonzima amekuwa akitawala sana mechi dhidi ya Azam FC na safari hii atakutana na nahodha msaidizi katika timu yake ya Taifa ya Rwanda, Mugiraneza. Tutaona mpira wa hali ya juu kama wachezaji hawatachezeana rafu za ubabe. TAMBWE, NGOMA & BUSUNGU, Washambuliaji hao watatu wataanza kwa pamoja katika safu ya mashambulizi ya Yanga. Tambwe amefunga magoli mawili, Busungu amefunga mara tatu wakati, Ngoma bado anatafuta goli lake la kwanza klabuni Yanga. Washambuliaji hao watatu wanaweza kufunga hata magoli mawili na zaidi katika gemu moja na kufanya hivyo mbele ya safu ya ulinzi ambayo haijaruhusu goli lolote katika gemu tatu mfululizo itakuwa ni jambo kubwa.
 Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Aggrey Morris na Paschal Wawa wamekuwa wagumu kupitika, labda ni kutokana na aina ya timu walizokutana nazo lakini kiu-alisia, Yanga wanapaswa kupambana hasa ili kuwa timu ya kwanza kufunga goli dhidi ya Azam katila michuano hii.
Safu yao ya mashambulizi imefunga magoli lakini bado wanakabiliwa na tatizo la upotezaji wa nafasi rahisi za kufunga magoli. Wawa amekuwa sababu kubwa ya ubora wa sasa katika safu ya ulinzi kutokana na uchezaji wake wa nguvu, uhamasishaji huku akiwa si mchezaji wa kufanya makosa yasiyotarajiwa.
Kapombe tayari amehusika katika magoli mawili ya timu yake. Mlinzi huyo wa kulia anaweza kuwa tatizo kwa Yanga kutokana na krosi-pasi zake, ni mchezaji asiyechoka kwenda mbele pale inapohitajika lakini uchezaji wake huo unaweza kuwa tatizo kwa kuwa, Ngoma si mchezaji wa kumuachia uhuru sana.
Nyoni ameendeleza kiwango chake kizuri na hivyo ataendelea kupangwa katika kikosi cha kwanza. Atamkabili, Kaseke ambaye amecheza kwa kiwango cha juu katika gemu nne zilizopita, wakati Wawa na Aggrey watakuwa macho kuhakikisha, Tambwe na Busungu hawapati nafasi ya kufunga. Nani mshindi wa gemu hii?. Ni mechi ngumu ila naipa Yanga asilimia 60 za kushinda kutokana na uzoefu wao wa michuano.

Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam

Yanga Vs Azam FC kagame Cup July 29, 2015

https://encrypted-tbn0.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcRBWxi4nnrll4wRu6b2XpjCWQOfIIHx9myY95WCGaDEHLxnkYw1 
 
YANGA SC
KIKOSI CHA YANGA LEO.
1.Ally Mustafa Mtinge "Barthez"
2.Juma Japhary Abdul
3.Mwinyi Hadji Ngwali.
4.Kelvin Patrick Yondani "Cotton"
5.Nadir Haroub Ally "Cannavaro"
6.Mbuyu Junior Twite.
7.Deus David Kaseke.
8.Haruna Niyonzima "Fabregas"
9.Donald Dombo Ngoma.
10.Amiss Jocelyn Tambwe.
11.Geofrey Mwashiuya "Lunyamila Jr"
BENCHI.
Deogratius Munishi "Dida"
Joseph Tetteh Zuttah.
Oscar Fanuel Joshua.
Pato Ngonyani.
Salum Abo Telela "Master"
Simon Happygod Msuva.
Malimi Busungu
Kikosi cha Azam FC leo. Mfumo 3-5-2
Manula Aishi
Agrey Morris
Kheri Abdallah
Pascal Wawa
Shomari Kapombe
Farid Mussa Shah
Himid Mao Mkamy
Jean Mugiraneza
Domayo Frank
John Bocco
Kipre Cheche
Sub 
1.Mwadini Ali
2.Metacha Mnatha
3.Said Morald
4.Ammy Ali
5.Abbas Mudathir
6.Didier Kavumbagu
7.Gadiel Michael