Kiongozi mmoja wa walimu hao aliambia BBC kwamba zaidi ya walimu miamoja sabini wameuawa mwaka huu.
Alituhumu maafisa wa serikali kwa kutoongeza juhudi za kuwalinda walimu na badala yake kujihusisha zaidi na siasa.
Wakati huohuo, Marekani imetuma vikosi vyake nchini Chad , nchi ambayo inapakana na Nigeria kama sehemu za juhudi zake kusaidia katika kuwatafuta wasichana waliotekwa nyara.
Source: BBC Swahili