Wednesday, 15 July 2015

UVCCM Zanzibar yajipanga katika uchaguzi mkuu 2015



Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi - CCM, SHAKA HAMDU SHAKA amesema Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi - UVCCM
Naibu Katibu Mkuu wa  Chama cha  Mapinduzi - CCM, SHAKA HAMDU SHAKA amesema Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi - UVCCM Kisiwani ZANZIBAR umejipanga vyema katika kuhakikisha CCM inanyakua baadhi ya majimbo Kisiwani  PEMBA katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwaka huu.

SHAKA amesema hivi sasa wameanza kujipanga kuhakikisha azma yao inafanikiwa kwa kuendelea kunadi vyema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi katika Kisiwa cha PEMBA.

Kuhusu uteuzi wa wagombea wa CCM ngazi ya Taifa SHAKA HAMDU  SHAKA amesema uteuzi huo umezingatia  vigezo vyote  vya sifa za wagombea ambao wote  wana uwezo mkubwa wa kuongoza Taifa. 

Hapo jana wanaCCM ZANZIBAR walifanya mapokezi ya kupongeza uteuzi wa nafasi ya Urais wa ZANZIBAR  kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi uteuzi ambao uliweza kupitishwa kwa asilimia mia moja na Mkutano Mkuu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM huko mjini DODOMA

No comments: