Wednesday, 5 March 2014

Ban apigia debe kilimo cha kaya kwa maendeleo vijijini


                                             Wakulima wa kaya
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ametoa wito kwa serikali ziwawezeshe wakulima wa kaya kwa kubuni sera zinazoweka mazingira stahiki kwa usawa na maendeleo endelevu vijijin, katika kuendeleza ujumbe wa 2014 ambao umetengazwa kuwa Mwaka wa Kilimo cha Kaya.

Hayo ni katika ujumbe wake kwa kongamano na maonyesho ya kimataifa kuhusu kilimo cha kaya mjini Budapest, Hungary, ambao umetolewa kwa niaba yake na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kilimo na Chakula, FAO José Graziano da Silva. 


Bwana Ban amesema kongamano hilo linatoa fursa ya kutambua mchango muhimu unaotolewa na wakulima wadogowadogo, jamii za wavuvi na wafugaji katika maendeleo endelevu na katika kutimiza mkakati wa kutokomeza njaa kupitia kwa mifumo endelevu ya chakula.

Amelipongeza pia kongamano hilo kwa kuangazia sehemu tatu za uendelevu, ambazo ni kiuchumi, kijamii na kimazingira, huku akiongeza kuwa mashamba ya kaya huleta pamoja sehemu zote tatu. Ameongeza kuwa moja ya vitu vinavyohitajika katika kuweka mifumo endelevu ya chakula ni kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na midororo ya kiuchumi.
 
          kilimo cha umwangiliaji 
Nchi kama Tanzania inahitaji kuweka mkanzo wa uwekezaji katika kilimo hasa maeneo mengi ya vijiji ambayo ni mhimu kwa kutoa ajira kwa wananchi walio wengi, kutoa chakula na kuleta ufanisi katika ukuzaji wa pato la nchi. mfano zaidi ya 80% ya watanzania wanategemea kilimo. "Lishe bora inatokana na uwekezaji katika kilimo"

                                       Kilimo cha Mahindi
Source: Redio ya Umaja Wa Mataifa