Saturday, 2 November 2013

NINI CHA KUFANYA UNAPOTENDEWA MABAYA NA MWENZA WAKO

Ili kuwa na uhusiano wenye amani kuna mambo muhimu ya kufanya. Kwani katika mahusiano kuna changamoto nyingi sana  unaweza kukuta kile anachokizungumza mwenza wako akiwa na wewe huku akikuonyesha mapenzi motomoto, na ukafikiri kuwa unapendwa kuliko kitu chochote lakini kumbe akitoka nje anatenda mambo mengine tofauti  na mabaya kabisa.

Kama kweli unataka amani ni vyema kujifunza kutenda mema. Tafakari na penda kufanya yale ambayo wewe mwenyewe ukiyatenda utayafurahia.Ukweli ni kwamba unaweza kufanya mambo kwa siri ukifikiria mwenzi wako hayajui kumbe yawezekana anajua na yeye akaamua kufanya hivyohivyo tena kwa siri yaani wote mkawa mnadanganyana.Hata kama mwenza wako anafanya mambo mabaya.

 Unachotakiwa kufanya ni kuendelea kumfanyia mazuri na si kutenda mabaya kwa kulipiza kisasi, kwani unapotenda mema yule mtenda mabaya atakosa amani na kuanza kutenda mazuri.Unapokwa katika mahusiano unatakiwa kujiona kama mtu mwenye deni la kumpenda mwenzako daima. KILA JAMBO LINAWEZEKANA NI MAAMUZI TU NA USHIRIKIANO BAINA YA WAPENDANAO.

Saturday, 28 September 2013

FURSA JIJINI MWANZA GOLD CREST HOTEL!!!!!

PICHA: Lulu akiwa jijini Mwanza kwenye semina ya FURSA. Apata nafasi ya kuzugumza na washiriki.

PICHA: Lulu akiwa jijini Mwanza kwenye semina ya FURSA. Apata nafasi ya kuzugumza na washiriki.
  • PICHA: Lulu akiwa jijini Mwanza kwenye semina ya FURSA. Apata nafasi ya kuzugumza na washiriki. 1
  • PICHA: Lulu akiwa jijini Mwanza kwenye semina ya FURSA. Apata nafasi ya kuzugumza na washiriki. 2
  • PICHA: Lulu akiwa jijini Mwanza kwenye semina ya FURSA. Apata nafasi ya kuzugumza na washiriki. 3
  • PICHA: Lulu akiwa jijini Mwanza kwenye semina ya FURSA. Apata nafasi ya kuzugumza na washiriki. 4
  • PICHA: Lulu akiwa jijini Mwanza kwenye semina ya FURSA. Apata nafasi ya kuzugumza na washiriki. 5
 
Tazama picha mbalimbali za mwadada Elizabeth Michael- LULU akiwa jijini Mwanza kwenye semina ya FURSA inayoandaliwa na kituo cha redio cha clouds FM.
Semina hiyo imeandaliwa kwa ajili ya wajasilimali mbalimbali mkoani humo waweze kuzitumia fursa mbalimbali zilizopo kwenye mazingira yao.
Lulu alikuwa mmoja wa wazungumzaji waalikwa wa semina hiyo.
28.09.2013 -  Tags:  Elizabeth Michael  lulu